KAMANDA WA POLISI APATA AJALI

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Arusha, Charles Mkumbo amepata ajali katika eneo la Mdori mkoani Manyara baada ya gari alilokuwa akilitumia kupasuka gurudumu 'tairi' ya nyuma na kupoteza uelekeo.


Hayo yamethibitishwa na mlinzi wa Kamanda Mkumbo (Bodyguard) wakati alivyokuwa anazungumza na mwandishi wa habari hii kwa njia ya simu ya RPC na kusema ni Kamanda Mkumbo amepata ajali hiyo ambapo ndani ya gari aliyokuwa akiitumia walikua watu watatu akiwemo msaidizi wake pamoja na dereva.

Kamanda Mkumbo amepelekwa katika hospitali ya Mount Meru mkoani humo baada ya kupata maumivu aliyokuwa nayo ya kichwa kutokana na ajali hiyo aliyoipata.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527