YANGA BALAA, YAIBAMIZA AZAM 2-1


Klabu ya Yanga leo imefanikiwa kupata ushindi magoli 2-1 dhidi ya Azam Fc , mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Azam complex leo jioni.

Azam ilikuwa ya kwanza kupata goli kupitia kwa mchezaji wake Shaaban Idd katka dakika ya tatu ya mchezo huo.

Dakika ya 30 Chirwa aliipatia Yanga bao la kusawazisha akiunganisha pasi mzuri aliyoipata kutoka kwa Ibrahim Ajib. 

Gadiel Michael aliipatia Yanga bao la pili na la ushindi katika dakika ya 44.

Matokeo ya mechi nyingine za ligi kuu leo ni

Mbeya City 0-0 Mtibwa sugar

Mwadui Fc 2-2 Njombe mji

Kagera sugar 0-0 Lipuli Fc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527