STEVE NYERERE AANIKA UGONJWA UNAOMSUMBUA



Msanii wa filamu, Steve Nyerere amefunguka na kusema kuwa ana wiki mbili yupo kitandani na kwamba ugonjwa unaomsumbua ni nyama kushikana na mifupa.

Amesema ugonjwa huo umemsababisha kushindwa kufanya kazi yoyote na kushindwa kutembea.

Muigizaji huyo amekiambia kipindi cha Enewz ya EATV kuwa anashangaa kwanini kila mtu anaongea lake kuhusu kuumwa kwake huku wengine wakifika mbali zaidi kwa kudai kwamba ameathirika.

“Watu wananifuatilia kutaka kujua hali yangu kwa sababu mimi ni mtu maarufu, ni jambo jema lakini kama kuna watu wamenitupia vitu vya ajabu naomba wanisamehe, mimi ni binadamu labda kuna namna watu nimewakosea,” amesema Steve. 

“Lakini nashangaa kuna watu wanadai imeathirika mmenipima, yaani kila mtu anaongea lake,”

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527