DARAJA LAPOROMOKA NA KUUA WATU 10

Watu kumi na mmoja wamefariki baada ya daraja lililokuwa likijengwa katika maeneo ya Chirajara kuporomoka nchini Colombia.


Maofisa wa Colombia wamesema watu waliofariki ni wafanyakazi wa Kampuni ya ujenzi ambao walikuwa kazini.


Maofisa hao wamesema wafanyakazi hao walikuwa wakishughulika na mfumo wa maji kwenye daraja wakati walipokutwa na umauti kwenye mradi huo uliopo kilomita 95 nje ya Gogota.


Taarifa zaidi zinasema watu tisa walifariki paelpale na mtu wa kumi baada ya kupelekwa katika hospitali ya karibu akiwa na majeraha makubwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527