Tanzia : ALIYEKUWA MUME WA IRENE UWOYA NDIKUMANA HAMAD KATAUT AFARIKI DUNIA


Aliyekuwa Kocha Msaidizi wa Timu ya Soka ya Rayon Sports nchini Rwanda, Hamad Ndikumana Katauti amefariki dunia ghafla leo hii.

Kwa mujibu wa Afisa Habari wa Rayon Sports Gakwaya Olivier, amesema kifo cha Ndikumana kilisababishwa na ugonjwa wa moyo.

“Alisikia maumivu makali kifuani akaomba soda ya baridi wakamletea na alipomaliza kunywa tu kidogo akatapika na akaishiwa pumzi na ndipo akakata kauli,” alisema Olivier na kuongeza kwamba bado wanasubiri uchunguzi wa madaktari.

Ndikumana ambaye amewahi kucheza soka Tanzania akiwa na klabu ya Stand United, amewahi kuwa mume wa muigizaji Irene Uwoya na wana mtoto mmoja.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527