RAIS MTARAJIWA WA ZIMBABWE AWASILI MJINI HARARE

Rais mtarajiwa wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa amerudi nchini humo kutoka Afrika Kusini.

Anatarajiwa kutoa hotuba yake katika makao makuu ya chama cha Zanu-PF mjini Harare.

Awali Mnangagwa amekutana na rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma.

Bwana Zuma alitarajiwa kuwasili atika mji mkuu wa Harare leo ili kuwa mpatanishi wa mgogoro uliokuwa ukiendelea lakini akafutilia mbali zaiara hiyo baada ya rais Mugabe kujiuzulu.

Ofisi ya rais Zuma ilituma ujumbe wa Twitter wa picha za mkutano wao.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527