Picha : AJALI YA LORI NA NOAH YAUA WATU WATANO MKOANI KILIMANJARO


 Habari kutoka Wilayani Hai ,mkoani Kilimanjaro watu watano wamepoteza maisha na wengine wanne wakijeruhiwa baada ya lori kugongana uso kwa uso na Noah maeneo ya kikavu kwa Sadala.

Daktari wa zamu hospitali ya wilaya ya Hai,Agness Temba amesema amepokea miili ya watu wa tano.

Amesema miili ya marehemu imehifadhiwa katika hospitali ya wilaya ya Hai, na majeruhi wamekimbizwa katika hospitali ya Rufaa ya KCMC Moshi.





Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527