MKIKITA WASAINI MKATABA NA FARMSTER YA ISRAEL KUTAFUTA MASOKO YA MAZAO YA MKULIMA KWA MTANDAO WA SIMU

 Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (Mkikita), Adam Ngamange (kushoto) na Ofisa Mtendaji wa Kampuni ya Farmster ya Israel, Adam Abramson wakitia sahihi mkataba wa makubaliano ambapo Farmster itatoa huduma za upatikanaji wa masoko ya mazao na bidhaa za wakulima wanachama wa Mkikita kwa njia ya mtandao wa simu. Hafla hiyo ilifanyika viwanja vya Camp of Good Hope, Goba  jijini Dar es Salaam.



Abramson ambaye ni mwasisi wa Farmster aliwaelezea waalikwa waliofika kwenye hafla hiyo jinsi  jinsi ya kujiunga na mtandao huo kwa kutumia simu za smart na za kawaida yaani 'vitochi' ambapo mkulima huingiza namba ya simu 0623 753016 kwa kutuma neno Jambo.


Mkulima atapaswa kutaja jina lake, eneo analoishi yaani shamba lilipo, analima zao gani, heka ngapi na anatarajia kuvuna lini na kwa kiasi gani ambapo huunganishwa moja kwa moja kwa mteja atakayejadiliana bei ya kuuzia.


Wakala Mkuu kati ya Mkulima na Mnunuzi utakuwa ni Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (MKIKITA), kitendo ambacho kitasaidia sana kuuvunja mtandao wa madadali wanaosumbua na kuwaibia wakulima.


Wakulima waliohudhuria hafla hiyo walionekana kufurahishwa na ujio wa teknolojia hiyo mpya na ya kisasa itakayowarahisishia wakulima kupata masoko mazao yakiwa shambani.IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG

 Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (Mkikita), Adam Ngamange (kushoto) akibadilishana hati za makubalino baada ya kutiliana sahihi mkataba  na Ofisa Mtendaji wa Kampuni ya Farmster ya Israel, Adam Abramson ambapo Farmster itatoa huduma za upatikanaji wa masoko ya mazao na bidhaa za wakulima wanachama wa Mkikita kwa njia ya mtandao wa simu

 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (Mkikita), Dk. Kissui S. Kissui (kushoto), akimpongeza Ofisa Mtendaji wa Kampuni ya Farmster ya Israel, Adam Abramson kutiliana sahihi mkataba wa makubaliano na Mkurugenzi Mtendaji wa  Mkikita, Adam Ngamange (katikati) ambapo Farmster itatoa huduma za upatikanaji wa masoko ya mazao na bidhaa za wakulima wanachama wa Mkikita kwa njia ya mtandao wa simu. 

 Abramson akifafanua jambo wakati wa hafla hiyo

 Akionesha namba ya kujiunga na mtandao huo

 Wanachama wa Mkikita wakisikiliza wakati mtalaamu huyo akiwaelezea faida mbalimbali atakazopata mkulima kwa kutumia mtandao huo

 Abramson akionesha eneo alipo mmoja wa wakulima aliyejiunga na mtandao huo

 Mkulima akipata maelezo kutoka kwa Abramson

 Wakulima wakiwa makini kumsikiliza mtalaam huyo

 Dk. Kissui ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mkikita akiwatambulisha wakurugenzi wa bodi ya Mkikita.

 Wakulima wanachama wa Mkikita wakiwa katika hafla hiyo



 Maofisa wa Mkikita wakiwa katika tukio hilo

 Dk Kissui akifafanua jambo wakati wa hafla hiyo

 Mkurugenzi Mtendaji wa Mkikita, Adam Ngamange akielezea jinsi walivyojipanga kumkwamua mkulima wa Tanzania kwa kutumia mbinu ama njia za kisasa kutafuta masoko



 Mapochopocho yakitayarishwa na wafanyakazi wa Spicy Catering kwenye viwanja mwanana vya Camp of Good Hope, Goba, Dar





 Wakulima wakionesha ishara ya kufurahishwa na  Mkikita kujiunga na Farmster

 Meneja Uhusiano wa Mkikita, Neema akijadiliana jambo na mmoja wa wanachama wa Mkikita

 Mkurugenzi Mtendaji wa Mkikita na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bima ya B&B Insurance Brokers Limited, Basil Bintamanyire wakitiliana sahihi kuingia mkataba ambapo kampuni hiyo ya Bima itakuwa washauri wa Mkikita kuhusu masuala yote ya bima katika kilimo na ufugaji



 Baadhi ya wakulima wakiwa katika hafla hiyo



 Msosi




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527