Aliyekuwa Mbunge wa Singida Kaskazini (CCM), Lazaro Nyalandu amemtembelea Waziri Mkuu wa zamani na mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa ofisini kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Nyalandu aliyejiondoa CCM wiki iliyopita leo Jumanne Novemba 7,2017 amemshukuru Lowassa kwa kuonyesha njia kwa wengine kuwa kuna maisha nje ya CCM.
“Mzee wangu nimekuja kujitambulisha na kusema asante kutufungulia mlango,” amesema Nyalandu katika taarifa iliyotolewa na ofisi ya Lowassa.
Kwa upande wake, Lowassa aliyetoka CCM mwaka 2015 amemkaribisha Nyalandu upinzani akisema, “Nimefarijika kuja huku karibu sana tushirikiane na kwa hakika 2020 tutavuka daraja.”
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin