AUAWA KWA KUPIGWA RISASI AKISAFIRISHA NG'OMBE ANAYEAMINIWA KUWA NI MUNGU

Viongozi wa kijamii katika mji wa Rajasthan nchini India wanasema mtu mmoja ambaye ni muislam ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wanaoamini ng'ombe kuwa mungu wao.

Ummar Khan alikua akisafirisha ng'ombe yeye na mwenzake katika kitongoji cha Alwar wakati walipovamiwa na wahindu.

Wanasema kwamba mwili wa kijana huyo ulitupwa karibu na reli kuharibu ushahidi.

Polisi katika mji wa Rajasthan wameanzisha upelelezi juu ya tukio hilo.Umekuwa ni utamaduni wao tokea enzi na enzi

Wahindu huamini kuwa ng'ombe ni mungu kwao na huwachukulia kwa namna ya upekee sana.

Zaidi ya watu kumi wameuawa tokea mwaka 2015 kwa sababu kama hizo.
Chanzo-BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527