BENKI YA TPB YATOA MSAADA WA MASHUKA NA VYANDARUA KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA KAHAMA


Mkurugenzi wa uendeshaji na Teknohama kutoka makao makuu ya benki ya Posta (TPB) Jema Msuya (wa pili kutoka kushoto) akikabidhi mashuka na vyandarua kwa afisa takwimu wa halmashauri ya mji wa Kahama Flora Sangiwa ambaye alimwakilisha mkurugenzi.
*****
Takriban wagonjwa elfu 24 hadi elfu 30 wanapokelewa kila mwezi katika hospitali ya Mji wa Kahama mkoani Shinyanga idadi ambayo inatajwa kuwa ni kubwa ukilinganisha na miundombinu ya hospitali hiyo.

Hayo yamesemwa leo na Mganga mfawidhi wa hospitali hiyo, Dr. Fredrick Malunde wakati akipokea msaada wa mashuka 100 na vyandarua 50 vyenye thamani ya shilingi milioni mbili vilivyotolewa na Benki ya TPB.

Amesema kutokana na wingi wa wagonjwa wadau wanapaswa kuguswa kutoa misaada ya vifaa ili kukabiliana na changamoto hizo.

Naye Mkurugenzi Uendeshaji na Teknohama kutoka makao makuu ya Bank ya TPB Jema Msuya amesema Benki hiyo itaendelea kusaidia kuchangia miradi ya maendeleo katika sekta mbalimbali huku akiwaomba wadau wengine wajitokeze kusaidia sekta za afya.

Afisa Takwimu wa Halmashauri yam Mji wa Kahama, Flora Sangiwa ambaye amemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo amesema halmashauri hiyo itaendelea kuthamani michango ya wadau wa maendeleo na kuipongeza benki ya TPB kwa msaada huo.

ANGALIA MATUKIO KATIKA PICHA

Wafanyakazi wa Benki ya TPB wakisomba vyandarua na mashuka mara baada ya kufika katika hospitali ya wilaya ya Kahama.
Afisa mawasiliano wa Benki ya TPB Moves Moses akiwaonyesha waandishi wa habari ubora wa vyandarua walivyovitoa katika hospitali hiyo. 
Wafanyakazi wa Benki ya TPB wakiteta jambo muda mchache kabla ya kuanza kwa zoezi la ugawaji wa mashuka na vyandarua.


Mganga mfawidhi wa Hospitali ya wilaya ya Kahama Fredrick Malunde akiteta jambo na meneja wa tawi la TPB Kahama wakati wa makabidhiano ya vifaa hivyo.
Baadhi wa wahudumu wa afya katika hospitali ya wilaya ya kahama wakiwa katika eneo la tukio kushuhudia utolewaji wa msaada huo wa mashuka na vyandarua.


Waandishi wa habari na baadhi ya viongozi wa hospitali ya wilaya ya Kahama na wafanyakazi wa TPB wakifuatilia zoezi la utolewaji wa vifaa hivyo.




Mganga mfawidhi wa hospitali ya wilaya ya Kahama Fredrick Malunde aliyesimama akitoa tathmini ya hali ya hospitali kuhusu upungufu wa mashuka na vyandarua katika hospitali hiyo.




Baadhi ya wahudumu wa afya wakifuatilia zoezi la utolewaji wa vifaa hivyo katika hospitali ya wilaya ya Kahama.




Mganga mkuu wa hospitali ya wilaya ya Kahama Dr Lucas David aliyesimaam akitoa neno la shukrani kwa bank ya tpb katika zoezi la kupokea vifaa hivyo.





Afisa takwimu wa halmashauri ya mji wa Kahama Frola Sangiwa aliyemwakilisha mkurugenzi wa mji akitoa neno kwa niaba ya halmashauri.


Mkurugenzi wa uendeshaji na Teknohama kutoka makao makuu ya Benki ya TPB Jema Msuya akitoa neno wakati wa makabidhiano ya vifaa hivyo.





Afisa takwimu wa halmashauri ya mji wa Kahama Frola Sangiwa aliyemwakilisha mkurugenzi wa mji akimkabidhi bahasha ya neno la shukrani Jema Msuya kutoak Benki ya TPB


Picha pamoja baada ya makabidhiano ya vifaa hivyo katika hospitali hiyo.




Mkurugenzi wa uendeshaji na Teknohama kutoka makao makuu ya Benki ya TPB Jema Msuya akiwa na mganga mfawidhi wa hospitali hiyo Dr. Fredrick Malunde wakimfunika mgonjwa na shuka jipya lililotolewa na benki ya TPB


Zoezi la kuwafunika wagonjwa likiendelea katika wodi ya wanawake.




Wafanyakazi wa Benki ya TPB wakitoka katika hospitali hiyo

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments