AKAMATWA AKISAFIRISHA MABOMU KWENYE MADUMU YA MAJI

Askari walimshtukia kijana huyo baada ya kupita kwenye vituo vitatu bila kusimama huku gari hilo likielekea kwenye kambi ya majeshi ya Umoja wa Mataifa kwa spidi kali.
Polisi mjini Kabul wamesema walitumia nguvu kubwa kumsimamisha kwa kulishambulia gari lake kwa risasi.

Wanajeshi wa UN nchini humo wamesema kuwa mabomu hayo yalichanganywa na mbolea na kuwekwa kwenye madumu huku mengine yakiwa kwenye maboksi ya nyanya hii ni baada ya kufanyiwa ukaguzi.

Hata hivyo, mpaka sasa hakuna kundi lolote la kigaidi lilitoa tamko juu ya tukio hilo.

Kwa mujibu wa UN nchini Afghanistan mamia ya raia wanauawa kila mwezi na makundi ya kigaidi ambapo kuanzia mwezi Januari hadi Septemba watu 1,584 wameshauawa kwenye matukio mbalimbali ya mashambulizi ya kigaidi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments