AHUKUMIWA JELA MIAKA 30 KWA KUBAKA NA KUMPA MIMBA MWANAFUNZI WA MIAKA 13

Mkazi wa Mtaa wa Mitandi Lindi Mjini, Mussa Hassan (35) amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela na kulipa fidia ya Sh1 milioni, baada ya kukutwa na makosa ya kubaka na kumpa mimba mwanafunzi wa miaka 13 aliyekuwa anasoma darasa la sita.


Akisoma hukumu hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa, Erasto Philly alisema Mahakama imemtia hatiani mshtakiwa kutokana na ushahidi uliotolewa na shahidi namba moja katika kesi hiyo ambaye ni mwanafunzi.


Hakimu Philly alisema mshtakiwa alitenda makosa hayo Agosti 2017, kwa kumbaka na kumpa mimba mwanafunzi huyo.


Awali, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Emmanuel John aliiomba Mahakama kutoa adhabu kali kutokana na mshtakiwa kutenda kosa la kinyama tofauti na umri wake ikilinganishwa na wa binti.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments