WANAFUNZI 24 WAZAMA ZIWA VICTORIA

Wanafunzi 24 wa shule ya msingi Butwa iliyopo kata ya Izumacheli, mkoani Geita wamezama katika kisiwa cha Butwa katika Ziwa Victoria walipokuwa wanatoka shuleni.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mkuu wa wilaya ya Geita, Herman Kapufi, kati ya wanafunzi hao 24 waliozama wakiwa ndani ya mtumbwi, 21 wameokolewa jana usiku lakini watatu bado wanatafutwa.

Taarifa zinaeleza kuwa ajali hiyo ilitokea jana saa 10 jioni baada ya mtumbwi huo kupinduka katika Ziwa Victoria.


Hata hivyo, kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Geita ikiongozwa na mkuu wa mkoa wa Geita, Ezekiel Kyunga imeelekea kwenye eneo la tukio kushiriki zoezi la uokoaji.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527