EMMANUEL MBASHA AELEZA JINSI FLORA MBASHA ALIVYOSALITI NDOA NA KUZAA NJE YA NDOA

Muimbaji wa nyimbo za injili madam Flora (Zamani Flora Mbasha) amekiri kupata mtoto nje ya ndoa yake na aliyekuwa mume wake Emmanuel Mbasha ambaye pia ni muimbaji wa nyimbo za injili. Imefahamika.


Hilo limefichuliwa leo na aliyekuwa mumewe, Emmanuel Mbasha, alipokuwa kwenye kipindi cha Kikaangoni kinachorushwa kupitia ukurasa wa facebook wa EATV .


Ishu hiyo imeibuka baada ya mmoja kati ya watu waliouliza maswali, kumtaka Mbasha kunyoosha maelezo kuhusu mtoto wa pili wa Flora kama ni wake ama la, na ndipo Mbasha akaweka wazi kuwa mtoto yule si wake, na Flora mwenyewe alishakiri suala hilo.


Mbasha amesema kuwa, Flora alikiri suala hilo hivi karibuni wakiwa katika harakati za kuachana kwa mujibu wa sheria mahakamani, ambapo ilipofika wakati wa kutaja idadi ya watoto aliozaa naye, Flora alimtaja mtoto mmoja pekee ambaye ni Elizabeth (akiwa ni mtoto wao wa kwanza)


"Yule mtoto siyo wangu, hata katika hati ya mashitaka ya kuachanishwa na mahakama, yeye mwenyewe Flora kwa mkono wake akiwa na wanasheria wake, aliandika kwamba kwa kipindi chote ambacho aliishi na mimi alibahatika kupata mtoto mmoja pekee ambaye ni Eliza, kwahiyo mpaka hapo unajua kabisa kwa hapa imeshakula kwangu, ni kitu ambacho kinauma sana, lakini kila mtu na ujasiri wake" Alisema Mbasha.


Kuhusu uamuzi aliouchukua baada ya kuthibitishiwa hilo, Mbasha amesema "Nilipojua siyo wa kwangu nilikaza moyo, nikasema basi Mungu ana makusudio yake, lakini kama ningeichukulia kibinadamu, ningeushangaza ulimwengu na dunia"


Kuhusu uwezekano wa kurudiana na Flora, Mbasha amesema kuwa yeye na Flora mapenzi yao yalishakwisha kutokana na mwenza wake huyo kuamua kuanza maisha mapya na kumuacha yeye.


Wakati akijibu moja ya swali kutoka kwa shabiki aliyetaka kujua ni jambo gani lililopelekea yeye kuachana na mkewe Flora Mbasha ndipo hapo Mbasha alifunguka na kusema yeye hajamuacha mkewe, bali mkewe ndiye alimuacha yeye kwa kumsaliti na mtu mwingine kwa sababu za kimaslahi na tamaa kutokana na umaarufu uliowafanya waweze kuonana na watu wengi wenye uwezo wa kila aina kifedha ikiwemo viongozi wa serikali na wafanyabiashara.


"Mimi siwezi kusema nilimuacha mke wangu, bali mwenzangu tayari alikuwa na maisha mengine yaani tayari alikuwa na njia zake na alishakuwa amefanya maamuzi na kuamua kwenda na njia ambayo yeye aliona ni sahihi na kuendelea na maisha yake. Hivyo alinisaliti kwa sababu ya maslahi na kwenda kwingine ambako anaona ni sehemu sahihi kwake" alisema Mbasha


Msanii huyo anakiri kuwa kitendo hicho kilimuumiza sana na kumtesa lakini yeye alimtumaini na kumuomba Mungu kwani hakutaka kuvuta bangi, au kunywa pombe ili kuondokana na 'stress' bali alimuomba Mungu na Mungu alimsaidia kupita katika kipindi hicho kigumu.


Kuhusu kuoa tena, Mbasha amesema hana mpango wa kuoa kwa kuwa hajapata mtu wa kuoa, hivyo ameamua kubaki 'single boy'


Katika hatua nyingine amesema hawezi tena kwenda wala kuhudhuria ibada katika Kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na Askofu Josephat Gwajima baada ya kukosana na mtu mmoja ambaye hajamuweka wazi, na kwamba sasa amerudi kwenye kanisa lake la zamani, la EAGT.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527