MTIBWA SUGAR WAIZUIA YANGA KUONGOZA LIGI KUU LEO


Siku moja baada ya wekundu wa Msimbazi Simba kucheza mchezo wao wa 24 wa Ligi Kuu Vodacom Tanzania bara dhidi ya Mbeya City na kulazimishwa sare ya 2-2, leo March 5 2017 ilikuwa zamu ya watani wao wa jadi Yanga kucheza dhidi ya Mtibwa Sugar katika uwanja wa Jamhuri Morogoro.


Yanga ambao walikuwa na point 52 mchezo wao wa leo kama wangepata ushindi wangekuwa sawa kwa point na watani wao wa jadi Simba lakini Yanga wangepata nafasi ya kuongoza Ligi hiyo kwa kuwa na idadi kubwa ya magoli kuliko Simba.

Kutoka katika uwanja wa Jamhuri Morogoro Yanga wamelazimishwa sare tasa 0-0 dhidi ya Mtibwa Sugar, licha ya kupata penati ambayo ilipigwa na Simon Msuva na kukosa penati hiyo, Simba sasa anaendelea kuongoza kwa tofauti ya point mbili dhidi ya Yanga ambao wana point 53.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527