GAZETI LA MWANAHALISI LAMUANIKA PAUL MAKONDA....LIMEWEKA KAMBI KOLOMIJE


Nyumba aliyokulia Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (Daudi Bashite)

KILA pembe ya kijiji cha Koromije, Wilaya ya Misungwi, pamoja na viunga vya jiji la Mwanza Paul Makonda, Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam anatajwa na kufahamika kama Daudi Albert Bashite, wanaandika Waandishi Wetu.


Wanaomtaja kwa jina hilo ni wanakijiji, ndugu zake, wanafunzi aliowahi kusoma nao pamoja na watu waliowahi kumshuhudia akifanya kazi kama kondakta.


Gazeti la MwanaHALISI baada ya uchunguzi wake wa kina uliohusishwa kutuma timu ya maripota wake jijini Mwanza, wanakuletea habari kamili inayofichua ukweli wa sakata hilo huku mama na baba wa Makonda, shangazi yake na wanafunzi waliowahi kusoma naye wakiwa wamehojiwa.
Shule ya Msingi aliyosoma Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam

Chanzo: Mwanahalisi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527