Picha 50: KIKAO KIKUBWA CHA KAMATI YA MAANDALIZI YA MKUTANO MKUU NA SHEREHE ZA KUMUAGA ASKOFU WA KANISA LA AICT DR. JOHN NKOLA


Jumamosi Februari 18,2017,kumefanyika kikao cha kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu na sherehe za kumuaga Askofu wa Kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT) Dayosisi ya Shinyanga Dkt.John Kanoni Nkola ambaye anastaafu uaskofu mwezi Agosti mwaka 2017. 


Kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa NSSF mjini Shinyanga ambapo mamia ya wachungaji,viongozi na waumini wa kanisa hilo dayosisi ya Shinyanga ambapo mgeni rasmi alikuwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mheshimiwa Josephine Matiro. 

Mnenaji mkuu katika kikao hicho alikuwa Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala. 

Akizungumza wakati wa kikao hicho Askofu Dkt. Makala aliwapongeza viongozi wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga wakiongozwa na Katibu mkuu wa kanisa hilo,Mchungaji Jakobo Mapambano kwa kuandaa sherehe ya kumuaga Askofu Nkola ambaye amekuwa askofu wa Kanisa hilo tangu tarehe 24.10.1993. 

Askofu Makala alitumia fursa hiyo kuwaonya waumini wa kanisa hilo kutokuwa na tamaa ya madaraka ya uongozi kwa nafasi itakayoachwa na Askofu Nkola hili kuepuka vurugu zinazoweza kujitokeza na kusisitiza kuwa ni vyema kiongozi atakayeziba nafasi hiyo apatikane kwa utaratibu unaotakiwa.

Akizungumza wakati wa kufungua kikao hicho,mgeni rasmi,Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro alitumia fursa hiyo kuwakumbusha viongozi wa dini kuongeza nguvu katika kueneza neno la mungu kwani watu wengi katika mkoa wa Shinyanga bado hawajamjua vyema mungu,wengi wao hawana dini.

Katika hatua nyingine Matiro aliwaomba viongozi wa dini kuiunga mkono serikali katika vita dhidi ya dawa za kulevya kwa kuhubiri watu waachane na vitendo.

Mwandishi mkuu wa Malunde1 blog,Kadama Malunde,alikuwepo katika kikao hicho…Ametuletea picha 50 za matukio yaliyojiri katika kikao hicho…Tazama hapa chini.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiwasalimia viongozi wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga wakati akiwasili katika ukumbi wa NSSF mjini Shinyanga kuhudhuria kikao chakikao cha kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu na sherehe za kumuaga Askofu wa Kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT) Dayosisi ya Shinyanga Dkt. John Kanoni Nkola ambaye anastaafu uaskofu mwezi Agosti mwaka 2017 .Kulia ni Makamu wa Askofu Dayosisi ya Shinyanga mchungaji Aaron Malyuta
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiwasalimia viongozi wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga akisalimiana na wachungaji wa kanisa la AICT
Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala 
Ndani ya ukumbi wa NSSF: Kushoto ni Katibu mkuu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Jakobo Mapambano,katikati ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga ,Josephine Matiro na Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala baada ya kuwasili ukumbini.
Maombi yakiendelea baada ya mgeni rasmi kuwasili ukumbini
Wajumbe wa kikao hicho wakisali ukumbini

Katibu mkuu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Jakobo Mapambano akitambulisha viongozi na wageni mbalimbali waliohudhuria kikao hichoAskofu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga, Dr. John Nkola.Hakuwepo wakati wa Kikao cha leo(Picha kutoka Maktaba ya Malunde1 blog

Katibu mkuu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Jakobo Mapambano alisema kikao hicho ni hatua ya awali ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu na sherehe za kumuaga Askofu wa Kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT) Dayosisi ya Shinyanga Dkt.John Kanoni Nkola ambaye anastaafu uaskofu mwezi Agosti mwaka 2017.
mkuu wa wilaya ya Shinyanga ,Josephine Matiro na Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala wakimsikiliza mchungaji Mapambano
Katibu mkuu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Jakobo Mapambano akiwapungia mkono wajumbe wa kikao hicho kutoka ndani na nje ya mkoa wa Shinyanga
Makamu wa Askofu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Aaron Malyuta akizungumza wakati wa kuthibitisha tamko la kuwakaribisha wajumbe na wageni katika kikao hicho
Wajumbe wakiwa ukumbini
Kwaya AICT Shinyanga wakiimba ukumbini
Kwaya ya AICT Shinyanga ikiimba
Wajumbe wakiwa ukumbini
wajumbe wa kikao hicho wakiwa wamesimama
Makamu wa Askofu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Aaron Malyuta akizungumza ukumbini
Kikao kinaendelea
Wajumbe wakiwa ukumbini
Kikao kinaendelea
Mwenyekiti wa kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu na sherehe za kumuaga Askofu wa Kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT) Dayosisi ya Shinyanga Dkt.John Kanoni Nkola,Erasto Kwilasa ambapo aliwaomba viongozi na waumini wa kanisa hilo kushirikiana naye katika kufanikisha mkutano huo na sherehe hizo
Kwaya AICT Kambarage ikiimba
Viongozi wa kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu na sherehe za kumuaga Askofu wa Kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT) Dayosisi ya Shinyanga Dkt.John Kanoni Nkola wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea ukumbini
Kushoto ni Katibu mkuu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Jakobo Mapambano na mkuu wa wilaya ya Shinyanga ,Josephine Matiro wakiwa wamesimama ukumbini
Viongozi wa Kanisa wakiwa ukumbini
Maombi yakiendelea kabla ya Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala
Maombi yanaendelea
Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala akizungumza wakati wa kikao hicho ambapo aliwataka waumini kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga kuyaenzi mambo mazuri yote yaliyofanywa na Askofu Dkt. John Nkola
Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala pia aliwahamasisha waumini wa kanisa hilo kudumisha upendo
Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala akizungumza ukumbini
Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala akiendelea kuzungumza
Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala akitoa neno ukumbini
Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala akiwa amesimama baada ya kumaliza kuzungumza
Meza kuu wakiwa wamesimama,wa kwanza kushoto ni mchungaji Samwel Njile kutoka Kanisa la AICT Pastoreti ya Masumbwe mkoani Geita
Kikao kinaendelea
Wajumbe wa kikao wakiwa ukumbini
Maombi yanaendelea
Makamu wa Askofu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Aaron Malyuta akizungumza ukumbini
Mchungaji Samwel Njile kutoka Kanisa la AICT Pastoreti ya Masumbwe mkoani Geita akiteta jambo na Katibu mkuu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Jakobo Mapambano
Wajumbe wa kikao 
Makamu wa Askofu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Aaron Malyuta akimkaribisha mgeni rasmi,mkuu wa wilaya ya Shinyanga ili azungumze na wajumbe wa kikao hicho
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza ukumbini ambapo aliwapongeza waumini wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga kuandaa sherehe maalum kumuaga Askofu Dkt. Nkola
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza ukumbini
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akisisitiza umuhimu wa kufikisha neno la mungu katika maeneo mengi zaidi ili wananchi wawe na hofu ya mungu
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza katika kikao hicho
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akisisitiza jambo
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiendelea kuzungumza
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akishikana mkono na mchungaji Mapambano baada ya kumaliza kuzungumza
Kushoto ni Katibu mkuu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Jakobo Mapambano,katikati ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga ,Josephine Matiro na Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala wakiwa ukumbini
Katibu mkuu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Jakobo Mapambano akimsindikiza Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala kutoka ukumbini baada ya kikao hicho kufunguliwa na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro.

Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527