MCHEKESHAJI MAARUFU MASELE CHAPOMBE AFUNGA NDOA..TAZAMA PICHA HAPA

Msanii wa vichekesho aliyejipatia umaarufu mkubwa kwa mtindo wake wa uchekeshaji akiigiza kama mlevi, Chrispine Lyogello, maarufu kama Masele au Chapombe.

Mwishoni mwa wiki hii ameaga ukapera baada ya kufunga ndoa na mchumba wake, Specioza Malick iliyofungwa katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Bikira Maria Consolata lililopo Mbezi Makabe jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya mashabiki walitoa maoni yao kuhusu ndoa yao na kumshauri Mrembo huyo ajitayarishe kucheka zaidi na wakati huohuo awe na ubavu wa kutenganisha kazi ya Masele na maisha halisi.


Muigizaji Masele, amekuwa msanii wa kwanza kufunga ndoa ndani ya mwaka 2017.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527