Serikali yatangaza adhabu mpya kwa wala rushwa

Serikali imeeleza dhamira yake ya kuongeza adhabu kwa watu wanaobainika kuhusika na rushwa ili wawe wanalipa fidia ya hasara iliyojitokeza mbali na kutumikia kifungo.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mh. Angellah Kairuki amesema kuwa adhabu zinazotolewa kwa wala rushwa ni ndogo ikilinganishwa na hasara wanayoisababishia serikali, hivyo marekebisho ya sheria hizo itamtaka mlarushwa kulipa fidia ya hasara iliyojitokeza

Akiongea na waandishi wa habari, mara baada ya kuzinduliwa kwa wiki ya kupokea malalamiko ya wananchi, katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, Mhe Angella amesema serikali itahakiki mali za viongozi wa serikali wapatao 500 na kuwataka wananchi kujitokeza kuhakiki mali za viongozi wao pamoja na kutoa taarifa ambazo serikali haikufanikiwa kuzipata.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527