MSANII WA MUZIKI WA INJILI SBJ AZUA BALAA NA WIMBO WA 'YESU NIPE NYONYO',ADAIWA KUDHALILISHA DINI

Gazeti la Kenya liitwalo taifa leo limeripoti kwamba bodi ya filamu kwenye nchi hiyo imehuzunishwa na Msanii wa muziki wa Injili SBJ kuimba wimbo wa Injili ambao unadhalilisha Imani.



Wimbo wenyewe unaitwa ‘Yesu nipe nyonyo‘ ambapo mkuu wa bodi hiyo Ezekiel Mutua alisema baadhi ya Waimbaji wa Kenya wamekosa maadili na kipaji cha kubuni au kutunga nyimbo nzuri zisizochafua hali ya hewa.


Alisema wimbo huo unaendelea kukaguliwa kwa sababu Wakenya wamekasirishwa: "Nashangaa sana mtu mzima anakaa chini na kuimba wimbo kama huu, Wasanii wetu wamejua kuwa kama hawaongei uchafu ama kutoa video za utata hawatasikilizwa wala kutazamwa na wanafanya hivyo ili wapate umaarufu”


Tayari bodi hiyo ilikua kwenye mipango ya kuwaandikia Youtube ambao ndio wanamiliki wa mtandao huo ili waiondoe hiyo video kwasababu bodi hiyo inayo mamlaka na katiba haitakubali Wasanii kutunga nyimbo za kudhalilisha imani.

Wimbo wenyewe huu hapa


Sikiliza/Tazama hapa Maelezo ya Bodi ya Filamu Kenya


Maoni ya Wadau kuhusu Wimbo wa Nyonyo

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527