WHATSAPP NA FACEBOOK SASA KUGAWANA NAMBARI ZA SIMU NA MAELEZO YA MTEJA



Kamishna wa mawasiliano nchini Uingereza anachunguza uamuzi wa programu ya WhatsApp wa kugawana data na kampuni ya facebook.

Data hiyo ya watumiaji wa WhatsApp itatumiwa kuvutia matangazo yanayoonekana na watumiaji wa mtandao wa facebook.

Itagawana nambari za simu na maelezo ya mara ya mwisho mteja kuingia katika akaunti yake ya WhatsApp na facebook.

Kamishna huyo amesema kuwa kwa kuwa mabadiliko hayo yataathiri watu wengi ,anataka maelezo zaidi kuhusu kile kitakachogawanywa kati ya huduma hizo mbili.

Kamishna Elizabeth Denham amesema kuwa watumiaji watakuwa na maoni tofauti kuhusu mabadiliko hayo.
 Via>>BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527