ORODHA YA WANAFUNZI 10 BORA WAVULANA MATOKEO DARASA LA SABA 2019...KANDA YA ZIWA BALAA

Baraza la Mitihani la Taifa la Tanzania (NECTA) limetangaza matokeo ya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi ambako mikoa ya kanda ya ziwa imeonekana kuongoza kwa kushika nafasi zote 10 bora kwa wavulana.

Katika matokeo hayo yaliotangazwa leo Jumanne Oktoba 15, 2019 nafasi ya kwanza hadi ya 10 katika orodha ya wavulana waliofanya vizuri zimeshikwa na wanafunzi kutoka katika mikoa ya kanda ya ziwa.

Nafasi ya kwanza imekwenda kwa Francis Gwaji kutoka shule ya Paradise ya mkoa wa Geita, wakati nafasi ya pili hadi ya nne ilichukuliwa na wanafunzi wa shule ya Graiyaki ya Mara ambao ni Victor Godfrey, Aziz Yassin na Goldie Hihayuma.

Nafasi ya tano imeshikwa na Daniel Daniel wa shule ya Little ya Shinyanga huku nafasi ya sita ikichukuliwa na Hilary Nassor wa shule Peaceland ya Mwanza.

Bado mikoa ya kanda ya ziwa imeendelea kutesa katika nafasi ya saba ambayo imeshikiliwa na Mbelele Mbelele wa Kwema Modern iliyopo Shinyanga, nafasi ya nane ikishikwa na Derick Lema wa shule ya Musabe mkoani Mwanza.

Namba tisa imechukuliwa na Athanas Sekuro wa Paradise ya Geita na dimba la wavulana kumi bora likifungwa na Aron Mabuga kutoka shule ya Kwema Modern ya Shinyanga.
 ANGALIA HAPA MATOKEO DARASA LA SABA 2019


Soma pia hizi↡↡↡↡
Breaking : ANGALIA HAPA MATOKEO YA MTIHANI DARASA LA SABA MWAKA 2019

KAULI YA UONGOZI WA SHULE YA LITTLE TREASURES BAADA YA KUSHIKA NAFASI YA NNE KITAIFA, YA KWANZA KIMKOA MATOKEO DARASA LA SABA 2019



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527