MAMA AUA WANAE WAWILI, AJINYONGA


Miili ya mama na wanaye

Amina Maketu mwenye umri wa miaka 34 amewaua watato wake wawili wenye umri wa miaka 9 na mwingine ana umri wa mwaka 1 na miezi 8 na kisha yeye mwenyewe kujinyonga huku chanzo cha tukio hilo ikiwa ni ugomvi wa ardhi uliotokea kwenye familia yake.

Akielezea tukuio hilo Kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma Michael Chilya, amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo Desemba 15,2022, katika mtaa wa Namanditi A, Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, huku sababu ya kutokea tukio hilo ikiwa ni ugomvi wa ardhi alikuwa anagombea yeye na ndugu zake ambapo marehemu ameacha ujumbe unaoeleza kuwa ameamua kujiua yeye na kuua watoto wake ili watoto wake wasipate tabu.

Akieleza kwa masikitiko makubwa Peter Komba ambaye ni mume wa marehemu amesema anasikitishwa na kitendo cha mke wake huyo kuwaua watoto wake kwani hakuwa na ugomvi naye licha ya kutengana naye.

Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments