KAGAME KUWANIA TENA URAIS RWANDA

Rais wa Rwanda, Paul Kagame,amesema atagombea tena urais katika uchaguzi wa mwaka 2024.

Katika mahojiano na televisheni ya Ufaransa, Bwana Kagame mwenye umri wa miaka 64 amesema kuwa "anaangalia uwezekano wa kugombea kwa miaka mingine 20".

"Uchaguzi ni kuhusu watu kuchagua," aliongeza.

Katika mwaka 2015 Bw Kagame alibadilisha katiba na hivyo kumruhusu kubakia mamlakani hadi mwaka 2034.

Katika uchaguzi wa mwishii miaka mitano iliyopita, takwimu rasmi zilionyesha kuwa alishinda kwa 99%ya kura – jambo ambalo wengi nje ya nchi hiyo walilipinga kuwa lisilowezekana.

Rais Kagame alitetea vikali rekodi ya haki za binadamuya Rwanda katika Mkutano wa Jumuiya ya Madola uliofanyika mwezi Juni mjini Kigali.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments