EDWIN SOKO AIBUKA KINARA WA TUZO YA HAKI YA KUPATA HABARI NA HAKI YA KUJIELEZA

Edwin Soko
Maria Sarungi

Kampuni ya SK Media imetoa tuzo haki ya kupata habari na haki ya kujieleza kwa mwaka 2021 / 2022, ambapo Edwin Soko ameibuka kuwa mshindi  wa kwanza wa tuzo hizo.

SK Media wametangaza tuzo hizo kwa kumtangaza Edwin Soko kuwa mshindi wa kwanza kwa kutetea kundi la waandishi wa habari wanaopata madhila  ya kukamtwa na Jeshi la polisi pamoja na mambo mengine yanayowagusa waandishi wa habari.


Mshindi wa pili wa tuzo hizo ni Mwanaharakati Maria Sarungi ambaye amepata tuzo kwa kupaza sauti za wananchi na kuiwezesha jamii kuwasiliana kurahisi kupitia mtandao wa Maria space kupitia mtandao wa twitter.

Mshindi wa tatu, wamegongana Boniface Jacob na Martine Mases ambao walifuatilia kesi ya Freeman Mbowe hatua kwa hatua kwa kutumia simu ya kiganjani.

Washindi hao watapata vyeti na zawadi nyingine mbalimbali.

 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments