Breaking : SPIKA WA BUNGE LA UGANDA AFARIKI DUNIA


Rais wa Uganda Yoweri Museveni ametangaza kifo cha Spika wa Bunge la Uganda, Jacob Oulanyah leo Jumapili “Alikuwa Kada mzuri nimechelewa kutoa taarifa ili Watoto wake wajulishwe kwanza”.

Kilichosababisha kifo cha Oulanyah hakijabainishwa lakini alikuwa amelazwa Hospitali nchini Marekani kwa zaidi ya mwezi mmoja na ilizua mjadala kwa Waganda ambao walidai iligharimu pesa nyingi sana za walipa kodi kumtibu.

Oulanyah alichukua kiti cha Spika wa Bunge la Uganda mnamo Mei 2021 na kabla ya hapo alikuwa Naibu Spika kuanzia 2011.

Kusafirishwa kwake hadi Marekani kwa matibabu kulizua mjadala miongoni mwa Waganda, ambao walidai kuwa iligharimu pesa nyingi sana za walipa kodi.


Bw. Oulanyah alichukua hatamu ya uongozi wa bunge la Uganda mnamo Mei 2021. Alikuwa naibu spika kuanzia 2011.

Alikuwa na sifa ya kuanzisha vikao vya bunge kwa wakati, na kila mara alitoa wito kwa wabunge kuimarisha ubora wa mijadala, kwa kujadili mambo waliyo na ufahamu wa kina.

Alikuwa mwanasheria na mwanasiasa wa muda mrefui. Aliwahi kuwa mbunge wa Eneo Bunge la Kaunti ya Omoro, kaskazini mwa nchi.

Bw. Oulanyah alikuwa miongoni mwa wanasiasa kutoka eneo hilo walioshiriki katika mazungumzo ya amani kati ya serikali ya Uganda na waasi wa Lord's Resistance Army walioongozwa na Joseph Kony miaka ya 2000.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments