AJIUA BAADA YA KUMJERUHI KWA KUMKATA MME WAKE AKIWA AMELALA

Mwanamke aliyetambulika kwa jina la Wande Emanuel (30) mkazi wa kijiji cha Sibwesa Wilayani Tanganyika Mkoa wa Katavi, amekutwa amejinyonga kwa kutumia kipande cha kitenge chake baada ya kudaiwa kumjeruhi kwa kumkata kichwani na kitu chenye ncha kali Mume wake anayefahamika kwa majina ya Dotto Enosi (35).

Akizungumza na Waandishi wa habari leo Machi 20, 2022 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi ACP Ali Makame Hamad amesema tukio hilo limetokea Machi 18, 2022 majira ya saa saa sita usiku katika kitongoji cha Kamlenga, kijiji cha Sibwesa.

ACP Hamad amesema chanzo cha tukio hilo ni ugomvi wa kifamilia uliosababishwa na shughuli za kilimo, ambapo imedaiwa kuwa Mwanamke alikuwa hataki kwenda shamba kulima hali iliyosababisha kutokea ugomvi huo uliomfanya Mwanamke huyo kumvizia Mume wake akiwa amelala na kumkata na kitu chenye ncha kali kichwani.

Chanzo - Site Digital Media 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments