SPIKA WA BUNGE AZITAKA ASASI ZA KIRAIA KUTUMIA TAKWIMU KULETA MAJAWABU KUKABILI CHANGAMOTO ZA WATANZANIA

 Asasi  za kiraia  (Azaki) zimetakiwa kufanya kazi kwa weledi,uadilifu,uzalendo kwa maslahi mapana ya taifa   ikiwa  ni pamoja na kutumia tafiti  na takwimu vizuri ambazo zitasaidia kutoa majawabu ya changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii ya watanzania.

Wito huo umetolewa leo jijini Dodoma na Spika wa Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai wakati wa ufunguzi wa wiki ya AZAKI (2021)  ambapo amesema asasi hizo hazina budi kutafuta fedha ndani na nje ya nchi  kwa ajili ya kuleta tija  na vipaumbele vya taifa .

Ndugai amezitaka asasi hizo kuwa na mwenendo wa kukosoa viongozi wa serikali lakini pia wana wajibu wa kuwapongeza hasa pale wanapofanya vizuri wanapotekelza majukumu yao kwa ajili ya maslahi ya watanzania wote.

Kwa upande wake rais wa  Taasisi ya uwezeshaji asasi za kiraia [Foundation For Civil Societt- FCS] Dkt,Stigmata Tenga amesema ipo haja kwa bunge kuleta mabadiliko na  kupitia upya sheria ,taratibu na miongozo ambayo inaziongoza asasi hizo  ili ziweze kushiriki vyema katika kutekeleza kazi zao na majukumu yao kwa maendeleo ya taifa.

Maonyesho ya wiki ya azaki kwa mwaka (2021) yanakwenda sambamba na kauli mbiu isemayo Azaki na Maendeleo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments