WAOMBAJI 68,019 WACHAGULIWA KUJIUNGA VYUO MBALIMBALI AWAMU YA KWANZA, DIRISHA AWAMU YA PILI KUFUNGULIWA AGOSTI 24
Monday, August 23, 2021
Waombaji 68,019 sawa na asilimia 73.2 ya waombaji 92,809, wamechaguliwa kujiunga katika Taasisi za Elimu ya Juu kwa kozi za Shahada za kwanza kwa mwaka wa masomo 2021/2022.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Tanzania (TCU) Profesa Charles Kihampa amesema ongezeko la waombaji limetokana na kuongezeka kwa wahitimu wa kidato cha sita.
Aidha Profesa Kihampa amesema dirisha la awamu ya pili la udahili linafunguliwa kesho Agosti 24,2021 mwaka huu hadi Septemba 6 mwaka huu, ili kutoa fursa kwa waombaji waliokosa nafasi kuomba katika awamu hiyo.
TCU imewataka waombaji kutuma maombi moja kwa moja katika vyuo, na kwa waombaji 35,548 waliochaguliwa chuo zaidi ya kimoja katika awamu ya kwanza ya udahili wanatakiwa kuthibitisha chuo kimojawapo katika vile walivyochaguliwa.
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin