UONGOZI SAO HILL WATOA MIEZI MIWILI KWA WAKANDARASI KUKAMILISHA UJENZI WA MABWENI

Kutoka kushoto Msimamizi wa mradi anayefuata ni Afisa Ugavi wa shamba John Keraryo na wa mwisho Mhifadhi Mkuu wa Shamba Juma Mwita Mseti akipata maelezo kutoka kwa wasimamizi haoMhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Sao Hill Juma Mwita  akipa maelezo wakati wa kukagua miradi ya ujenzi wa mabweni

Na fredy Mgunda,Mufindi.

TFS kupitia Shamba la Miti Sao Hill linatekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika jamii inayozunguka shamba ikiwa ni pamoja na ujenzi wa mabweni katika shule za sekondari.


Wakati wa ukaguzi wa miradi hiyo Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Sao Hill Juma Mwita amesema lengo za ukaguzi wa miradi ni kuhakikisha miradi hii inakamilika kwa wakati kama ilivyokusudiwa.


Hata hivyo Mwita aliwataka wajenzi na wasimamizi wa miradi ya ujenzi wa mabweni kuhakikisha miradi hii inakamilika ndani ya miezi miwili ili wanafunzi wanapofungua shule mwezi Januari mabweni hayo yaweze kutumika.


"Lengo la mabweni haya ni kusaidia watoto wetu wa kike ili wakae mahali salama wakiwa shuleni na hii itasaidia sana wanafunzi hao kusoma katika mazingira mazuri."Alisema Mhifadhi Mkuu wa Shamba


Mwita aliongeza kuwa TFS inasaidia jamii katika miradi mbalimbali ikiwa ni sehemu ya kuonyesha shukrani na kuwakumbusha wananchi kuendelea kulinda misitu iliyopo kwa faida mbalimbali zinazoonekana.


Naye Mwalimu Paul Msukwa kutoka Shule Sekondari Ihanu alisema kuwa mabweni haya yatawasaidia sana wanafunzi wa kike kuondokana na changamoto zinazowakabili na itasaidia ufaulu kupanda.


"Mabweni haya mawili yaliyokaguliwa ambayo yapo katika Shule ya Sekondari Luganga na Ihanu yatakuwa na uwezo wa kuchuka wanafunzi 160 kwa wakati mmoja" alisema

KAWAIDA:

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments