RAIS WA ZANZIBAR, DK HUSSEIN ALI MWINYI KULIFUNGUA BARAZA LA WAWAKILISHI LEO
Wednesday, November 11, 2020
Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Ali Mwinyi leo anatarajiwa kulifungua Baraza la Wawakilishi kwa ajili ya kuanza kazi rasmi kwa miaka mitano ijayo.
Taarifa iliyosomwa jana na Spika wa baraza hilo, Zubeir Ali Maulid ilieleza Rais atalizindua baraza leo saa 9 alasiri.
Taarifa hiyo ilieleza kwa mujibu wa utaratibu, baraza hilo ili lianze kazi ni lazima kuzinduliwa na rais baada ya kukamilika kwa baadhi ya shughuli za kikatiba za baraza. Miongoni mwa shughuli hizo ni pamoja na kuchaguliwa kwa Spika na Naibu wake.
Kazi nyingine ni kuapishwa kwa wajumbe wa baraza waliohudhuria mkutano huo wakiwemo kutoka majimboni, wa viti maalum pamoja na walioteuliwa na Rais.
Katika kikao cha jana, kulifanyika uchaguzi wa Naibu Spika ambapo wajumbe wote 67 waliohudhuria walimchagua Mgeni Hassan Juma kwa kura zote za ndio.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin