WIZARA YA KILIMO YAGAWA VIFAA VYA TEHAMA VYA KUJIFUNZIA KWA VYUO 14 VYA KILIMO NCHINI

Na.Faustine Galafoni,Dodoma.

Katika kukabiliana na changamoto ya uhaba wa vitabu vya kujifunzia katika vyuo vya kilimo hapa nchini,Wizara ya kilimo imeamua kugawa vifaa vya kielektroniki  katika vyuo 14  vya kilimo   nchini vyenye thamani ya Tsh.Milioni 248.69.


Akizungumza na waandishi wa Habari Agosti,31,2020 jijini Dodoma katika hafla fupi ya ugawaji wa vifaa hivyo vya TEHAMA , Katibu mkuu Wizara ya Kilimo  Gerald Msabila Kusaya  amebainisha kuwa  tangu ateuliwe kuwa katibu Mkuu wa Wizara hiyo tarehe 5,Machi mwaka huu amebahatika kufanya ziara katika vyuo mbalimbali vya elimu ya kilimo  hapa nchini na kubaini changamoto ya uhaba wa vitabu hivyo na kuamua kununua vifaa vya kielekroniki kwa ajili ya kujifunzia .

“Baada ya kuona changamoto hiyo tulijadili na wadau tukaona namna nzuri ya kusoma  kwa njia ya kielekrtoniki  hivyo tumeamua kununua kununua vifaa mbalimbali hali itakayosaidia wanafunzi wetu ambao ni wataalam wa baadae wa kilimo kujifunza kwa njia ya mtandao na vifaa hivyo vikigharimu Tsh.Milioni 248.69 “amesema.

Aidha,Katibu mkuu huyo wa Wizara ya kilimo ametoa wito kwa wakuu wa vyuo vya kilimo kuhakikisha wanasimamia vinatumika vizuri na mara kwa mara ili kuwandaa  wataam wa kilimo wanaoendana na wakati.

Wakitoa neno la shukrani baada ya kupokea vifaa hivyo kwa niaba ya Wakuu wa vyuo 14 vya serikali,mkuu wa chuo cha Kilimo Mlingani Samson Cheyo pamoja na kaimu mkuu wa chuo cha Sukari [National Sugar Institute-NSI] Kilichopo Kilombero Mkoani Morogoro  Aloyce Kasmir wamesema vifaa hivyo vya TEHAMA vitarahisisha katika ufanisi wa kujifunza.

Baadhi ya vifaa vya TEHAMA vilivyotolewa ni pamoja na Rooter Machine,Kompyuta mpakato[laptop],Desk top,TV vikiwa na thamani ya Tsh.Milioni 248.69.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527