CCM YAFANYA UTEUZI WA WAGOMBEA UWAKILISHI KATIKA BARAZA LA WAWAKILISH ZANZIBAR

Kamati  Kuu Chama Cha Mapinduzi (CCM) imefanya uteuzi wa wagombea Uwakilishi katika Baraza la Wawakilish  Zanizbar katika majimbo 50 kwa kuzingatia uwezo, umahiri na utendaji wao.



Kikao cha kamati kuu kimefanyika jana Jumatatu tarehe 31 Aagosti 2020 jijini Dodoma chini ya Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli.

Mara baada ya kumalizika kwa kikao hicho, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Humphrey Polepole alitangaza majina ya walioteuliwa.


Polepole aliwataja waliopitishwa na majimbo kwenye mabano kuwa ni Zawadi Aamour Nasoro (Konde), Shamata Shahama Khamisi (Micheweni), Saidi Sale Salim (Tumbe), Tunu Mwalimu Masoud (Wingwi), Maliam Dhani Juma (Gando), Makame Said Juma (Kojani) na Othman Ali Khamis (Mtambwe).

Wengine ni Khamis Dadi Khamis (Pandani), Harus Said Suleiman (Wete), Shaibu Hassan Kaduara (Chake) Suleiman Masoud Makame (Chonga) Masoud Ali Mohammed (Ole), Bakari Hamad Bakari (Wawi), Suleiman Makame Ali (Ziwani), na Bahati Khamis (Chambani).

Mussa Kombo Mussa (Kiwani), Abdul Hussein Kombo (Mkoani), Mohammed Mgaza Jecha (Mtambile), Nadir Yussuf (Chaani), Juma Mkungu Juma (Kijini) na Mkwajuni ni Sulubu Kidongo Amour.

Pia wamo Abdul Abbas Wadi (Nungwi), Haji Omar Kheri (Tumbatu), Mtumwa Peya Yussuf (Bumbwini), Khalid Salum Mohammed (Donge), Asha Abdallah mussa (Mahonda), -Issa Haji Gavu (Chwaka), Haroun Ali Suleiman (Makunduchi), Paje- Dk. Soud Nahoda Hassan (Paje) na Mwanaasha Khamis Juma (Dimani).

Wengine ni Yussuf Hassan Iddi (Fuoni), Suleiman Haroub Suleiman (Kiembe Samaki), Ameir Abdallah Ameir (Mwanakerekwe), Ali Suleiman Ameir (Pangawe), Mudrik Ramadhan Soraga (Bububu), Machano Othman Said (Mfenesini), Hussein Ibrahim Makungu (Mtoni), Mihayo Juma Nhunga (Mwera), Hassan Khamis Hafidh (Welezo) na Rukia Omar Mapuri (Amani).

Miraji Khamis Mussa (Chumbuni), Jamaal Kassim Ali (Magomeni), Shaaban Ali Othman (Mpendae), Hamza Hassan Juma (Shaurimoyo), Ali Gullam Hussein (Jang’ombe), Nassor Salum Ali (Kikwajuni), Yahya Rashid Abdallah (Kwahani) na Malindi ni Mohammed Ahmada Salum



Polepole alisema Kamati Kuu imepitisha majina ya wawakilishi kundi la wanawake kwa Mkoa wa Kaskazini Pemba ambao ni Bihindi Hamadi Khamis, Chumu Kombo Khamis, na Farida Hamad Juma na Kaskazini Unguja ni Panya Ali Abdalah, Mwanajuma Kasim Makame na Fatma Hamza Mohamed.

Mkoa wa Kusini Pemba waliopitishwa ni Shadia Mohamed Suleimani, Zuhura Mgeni Othman na Zainab Omar Amir wakati Mkoa wa Kusini Unguja ni Salma Juma Bilal, Rahma Kasim Ally na Arafa Ali Yusuph.

Katika mkoa wa Magharibi Unguja, waliopitishwa ni Fatma Ramadhani Mandoba, Mwanaidi Kassim Mussa na Fatma Ali Akhmed na Mkoa wa Mjini Magharibi ni Saada Ramadhani Mwendwa, Mgeni Hassan Juma na Salma Abdi Ibada.

Kadhalika, Polepole alisema Kamati Kuu imewapitisha wawakilishi wanawake kwenye kundi la wenye ulemavu, ambao ni Mwantatu Mbaraka Khamis na Zainab Abdallah Salum na kundi la wasomi ni Riziki Pembe Juma,

Kwenye kundi la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) waliopitishwa ni Salha Mohamed Mwinjuma na Rahma Mbaraka Tahir na kwa upande wa wazazi ni Sabiha Filfili na Aza Januari Joseph.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527