RONALDINHO AACHILIWA HURU PARAGUAY


Ronaldinho Gaucho ameachiliwa kutoka kifungo cha nyumbani nchini Paraguay baada ya kufungwa kwa kumiliki paspoti ya kugushi.


Staa huyo wa zamani wa vilabu vya PSG, Barcelona na hata AC Milan, alikuwa anashikiliwa na mamlaka  za usalama za Paraguay pamoja na kaka yake ,Roberto de Asas ambaye anatambulika kama meneja wa nyota huyu wa zamani.

Nje ya soka Gaucho anatajwa kama mchezaji anayependa sana anasa na maisha ya ufahari yaliyochangia kutofanikiwa zaidi katika soka  na hata sakata hili la kuingia nchini Paraguay kwa hati ya bandia inaelezwa kuwa walikuwa wanakwenda katika uzinduzi wa moja ya kumbi za starehe ya usiku maarufu kama Cassino.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527