Picha : PATROBAS KATAMBI ASIMAMISHA MJI WA SHINYANGA AKICHUKUA FOMU KUGOMBEA UBUNGE SHINYANGA MJINI


Mgombea wa Nafasi Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini,Patrobas Katambi (CCM) akiwapungia mkono wananchi wa Shinyanga wakati akielekea katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini baada ya kuchukua Fomu ya Kugombea Ubunge kwa Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini,Geofrey Mwangulumbi.
***
Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mgombea wa Nafasi Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini,Patrobas Katambi (CCM) leo Jumamosi Agosti 22,2020 amechukua Fomu ya Kugombea Ubunge kwa Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini,Geofrey Mwangulumbi.


Katambi amechukua fomu ya kugombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kwa msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini akisindikizwa na Viongozi wa Chama cha Mapinduzi, Madiwani walioteuliwa kupeperusha Bendera ya CCM katika uchaguzi Mkuu 2020,Watia nia kugombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini mwaka 2020 na wanachama wa CCM.

Safari ya kuelekea katika ofisi ya msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini, Geofrey Mwangulumbi imeanzia katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini ambapo msafara wa wasindikizaji wakiambatana na mgombea ubunge Patrobas Katambi wakiwa kwenye magari na pikipiki walipita katika mitaa mbalimbali Mjini Shinyanga huku shughuli zikisimama kwa muda kupisha mgombea ubunge apite barabarani.

Mara baada ya kuchukua fomu,Katambi na msafara wake walielekea katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini ambapo Mgombea huyo wa Ubunge alitumia fursa hiyo kusalimiana na wanachama wa CCM na wananchi wa Jimbo la Shinyanga Mjini.

Akizungumza nje ya ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini wakati akisalimiana wanachama wa CCM na wananchi, Katambi amekishukuru Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumpitisha rasmi kupeperusha Bendera ya CCM Jimbo la Shinyanga Mjini katika uchaguzi Mkuu 2020 huku akisisitiza kuwa atakuwa Mbunge wa Kazi kuwaletea maendeleo ya kiuchumi na kijamii wananchi wa Shinyanga.

“Nilitoa sadaka nafasi yangu ya Ukuu wa wilaya kwa ajili ya wananchi wa Shinyanga. Naahidi kuwa nitawaheshimu watu wa dini zote na wasio na dini na niwaahidi utumishi uliotukuka na nitahakikisha nafanya kazi usiku na mchana,nitatumia nguvu zangu zote,akili zangu zote,maarifa yangu yote,mbinu zangu zote na maarifa yangu ili kuhakikisha ninawaletea maendeleo wananchi wa Shinyanga”,amesema Katambi.
ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Kulia ni Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini,Geofrey Mwangulumbi akimkabidhi Patrobas Katambi Fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini leo Jumamosi Agosti 22,2020. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kulia ni Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini,Geofrey Mwangulumbi akimkabidhi Patrobas Katambi Fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini leo Jumamosi Agosti 22,2020.
Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini,Geofrey Mwangulumbi akimsisitiza Patrobas Katambi kufuata sheria,kanuni na taratibu za uchaguzi wakati wa Kampeni za Uchaguzi.
Viongozi mbalimbali wa CCM wakiwa katika ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Abubakari Gulam na Mgombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi wakitoka katika ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mgombea wa Nafasi Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini,Patrobas Katambi (CCM) akiwa juu ya gari akielekea katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini baada ya kuchukua Fomu ya Kugombea Ubunge kwa Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini,Geofrey Mwangulumbi.
Mgombea wa Nafasi Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini,Patrobas Katambi (CCM) akiwa juu ya gari akielekea katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini baada ya kuchukua Fomu ya Kugombea Ubunge kwa Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini,Geofrey Mwangulumbi.
Mgombea wa Nafasi Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini,Patrobas Katambi (CCM) akiwa juu ya gari akielekea katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini baada ya kuchukua Fomu ya Kugombea Ubunge kwa Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini,Geofrey Mwangulumbi.
Mgombea wa Nafasi Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini,Patrobas Katambi (CCM) akisalimiana na wananchi mjini Shinyanga akielekea katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini baada ya kuchukua Fomu ya Kugombea Ubunge kwa Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini,Geofrey Mwangulumbi.
Mgombea wa Nafasi Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini,Patrobas Katambi (CCM) akisalimiana na wananchi mjini Shinyanga akielekea katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini baada ya kuchukua Fomu ya Kugombea Ubunge kwa Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini,Geofrey Mwangulumbi.
Mgombea wa Nafasi Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini,Patrobas Katambi (CCM) akisalimiana na wananchi mjini Shinyanga akielekea katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini baada ya kuchukua Fomu ya Kugombea Ubunge kwa Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini,Geofrey Mwangulumbi.
Mgombea wa Nafasi Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini,Patrobas Katambi (CCM) akisalimiana na wananchi mjini Shinyanga akielekea katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini baada ya kuchukua Fomu ya Kugombea Ubunge kwa Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini,Geofrey Mwangulumbi.
Mgombea wa Nafasi Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini,Patrobas Katambi (CCM) akisalimiana na wananchi mjini Shinyanga akielekea katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini baada ya kuchukua Fomu ya Kugombea Ubunge kwa Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini,Geofrey Mwangulumbi.
Msafara wa viongozi wa CCM na wanachama wa CCM ukielekea katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga baada ya Patrobas Katambi kuchukua fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Msafara wa viongozi wa CCM na wanachama wa CCM ukielekea katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga baada ya Patrobas Katambi kuchukua fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Msafara wa viongozi wa CCM na wanachama wa CCM ukielekea katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga baada ya Patrobas Katambi kuchukua fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mgombea wa Nafasi Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini,Patrobas Katambi (CCM) akiteta Jambo na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Abubakari Gulam baada ya kuwasili katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini.
Mgombea wa Nafasi Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini,Patrobas Katambi (CCM) akicheza muziki na viongozi na wanachama wa CCM baada ya kuwasili katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini.
Mgombea wa Nafasi Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini,Patrobas Katambi (CCM) akicheza muziki na viongozi na wanachama wa CCM baada ya kuwasili katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini.
Katibu wa Siasa na Uenezi CCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Said Bwanga akizungumza baada ya Mgombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi kuwasili katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini.
Katibu wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Agnes Bashemu akizungumza baada ya Mgombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi kuwasili katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini.
Mgombea Udiwani kata ya Ndala, Zamda Shaban ambaye ni mmoja wa waendesha bodaboda Mjini Shinyanga akizungumza baada ya Mgombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi kuwasili katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini.
Aliyekuwa mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini Salum Bandora Mirambo maarufu Salu Security akizungumza baada ya Mgombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi kuwasili katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini.
Aliyekuwa mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini Leonard Mapolu akizungumza baada ya Mgombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi kuwasili katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini.
Aliyekuwa mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini Manyama Jonathan Kifunda akizungumza baada ya Mgombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi kuwasili katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini.
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Abubakari Gulam akimkaribisha Mgombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi kusalimiana na wanachama wa CCM na wananchi wa Shinyanga.
Kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Abubakari Gulam akimtambulisha na kumkaribisha Mgombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi asalimiane na wanachama wa CCM na wananchi wa Shinyanga.
Kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Abubakari Gulam akimtambulisha na kumkaribisha Mgombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi asalimiane na wanachama wa CCM na wananchi wa Shinyanga.
Mgombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi akiwasalimia wanachama wa CCM na wananchi wa Shinyanga.
Mgombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi akiwasalimia wanachama wa CCM na wananchi wa Shinyanga.
Mgombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi akiwasalimia wanachama wa CCM na wananchi wa Shinyanga.
Wanachama na wananchi wa Shinyanga wakimsikiliza Patrobas Katambi.
Wanachama na wananchi wa Shinyanga wakimsikiliza Patrobas Katambi.
Wanachama na wananchi wa Shinyanga wakimsikiliza Patrobas Katambi.
Wanachama na wananchi wa Shinyanga wakimsikiliza Patrobas Katambi.
Mgombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi akiwasalimia wanachama wa CCM na wananchi wa Shinyanga.
Baba Mzazi wa Mgombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi, Dkt. Patrobas Katambi akiwasalimia wanachama wa CCM na wananchi wa Shinyanga.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527