MCHUJO MKALI WA KURA ZA MAONI KWA WAGOMBEA CCM WAANZA LEO


Mchakato wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wa kupata wagombea katika nafasi mbalimbali unaanza leo ambapo mikutano ya ngazi ya wilaya/majimbo itapiga kura za mapendekezo kati ya leo na kesho.

Upigaji wa kura unaoanza leo unahusisha kura za maoni za kuwapata wagombea katika nafasi za ubunge, uwakilishi, udiwani (Tanzania Bara) na usheha kwenye wadi visiwani Zanzibar.

Baada ya mikutano hiyo, Julai 30 kutakuwa na vikao vya kamati za siasa za majimbo kuwajadili wagombea na kutoa mapendekezo kwenye kamati za siasa za wilaya.

Vikao vya uteuzi kwa wagombea ubunge vitafanywa na Kamati Kuu (CC) ya Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM kwa Tanzania Bara na ujumbe wa Baraza la Wawakilishi ni Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu ya Taifa Zanzibar.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527