GRACE RUKANDA AJITOSA UBUNGE JIMBO LA KAHAMA MJINI


Baada ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuanza zoezi la Utoaji wa Fomu za kugombea nafasi za Ubunge, na Udiwani katika Wilaya ya Kahama yenye Majimbo Matatu ya Msalala,Ushetu na Kahama Mjini mwitikio wa wagombea wanawake umekuwa mkubwa ikilinganishwa na Uchaguzi wa mwaka 2015 ambapo mpaka sasa katika majimbo yote jumla ya wagombea wanawake 9 wamejitokeza kugombea nafsi hizo.

Bi Grace Rukanda, ambaye ni Mhasibu Mamlaka ya Maji safi na usafi wa mazingira Kahama(KUWASA) leo Julai 15,2020 amechukua fomu ya kuomba Ridhaa ya kuchaguliwa kugombea Ubunge katika Jimbo La Kahama Mjini kupitia Tiketi ya (CCM) ambapo mpaka sasa linawagombea saba Wanawake.#

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527