TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI YATANGAZA TAREHE YA UCHAGUZI MKUU TANZANIA


Tume ya Taifa ya Uchaguzi  (NEC) nchini Tanzania imesema, Uchaguzi Mkuu wa udiwani, ubunge na Urais wa Tanzania utafanyika Jumatano Oktoba 28, 2020.


Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Jumanne tarehe 21 Julai 2020, Mwenyekiti wa NEC, Semistocles Kaijage amesema Uchaguzi mkuu utafanyika October 28 Mwaka huu huku Kampeni zikitarajiwa kuanza August 26 hadi October 27, 2020.

Wakati huo huo Uteuzi wa Wagombea wa kiti cha Urais,Makamu wa Rais, Ubunge na Udiwani utafanyika August 25, 2020


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527