WHO: USHAHIDI TULIONAO UNAONESHA VIRUSI VYA CORONA VILITOKA KWA WANYAMA


Msemaji wa Shirika la afya duniani (WHO) Bibi Fadela Chaib jana kwenye mkutano na waandishi wa habari amesema, kwa mujibu wa ushahidi uliopo sasa, WHO inaamini kuwa virusi vya Corona vinatoka kwa wanyama.

“Ushahidi wote tulionao unaonesha kuwa virusi vya Corona vinatoka kwa wanyama, na havitokani na uingiliaji wa binadamu au kutengenezwa kwenye maabara.”

Vilevile amesema WHO inapambana na maambikizi ya virusi pamoja na uvumi. 

“WHO inapambana na kuenea kwa virusi vya Corona duniani, wakati huo huo inapambana na kuenea kwa habari feki duniani. Wakati virusi vipya kama virusi vya Corona vinapotokea, habari nyingine feki huenea kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.”- Alisema


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post