WAZIRI MKUU WA UINGEREZA BORIS JOHNSON ALIYEKUWA AMELAZWA ICU KWA CORONA ARUHUSIWA KUTOKA HOSPITALI

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson ametoka hospitali baada ya kupona virusi vya corona lakini atapumzika kwanza kabla ya kuanza kurejelelea majukumu yake.

Johnson, 55, alipelekwa St Thomas' hospital, mjini London, Jumapili - siku ya 10 baada ya kupatatikana na virusi hivyo.

Alikuwa katika chumba cha wagonjwa mahututi kwa siku tatu kabla ya kurejeshwa kwenye wodi ya kawaida Alhamisi.

Kulingana na taarifa iliyotolewa, Waziri Mkuu ataendelea kupumzika katika makazi ya Chequers.
Idadi ya watu waliokufa kwa virusi vya corona  nchini Uingereza inasemekana kupita 10,000 hadi kufikia Jumapili.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post