KESI YA PILI YA KIFO CHA EBOLA YARIPOTIWA KATIKA JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA CONGO


Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeripoti kesi ya pili ya kifo cha Ebola katika kipindi cha siku tatu baada ya nchi hiyo kupitia muda wa zaidi ya majuma sita bila ya kuripotiwa kesi mpya ya maambuzo ya Ebola.

Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza habari hiyo na kueleza kwamba, aliyeaga dunia kwa Ebola ni binti wa miezi 11 ambaye anasadikiwa kuambukizwa na mgonjwa aliyeaga dunia kwa maradhi hayo Ijumaa ya juzi huko katika mji wa Beni.

Hayo yanaripotiwa katika hali ambayo, leo amhuri ya Kidemokrasia ya Congo ilitarajiwa kutangaza rasmi kumalizika kabisa ugonjwa huo katika nchi hiyo ambao umeua zaidi ya watu 2,200.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post