MBOWE ASHAURI KUUNDWA KWA KIKOSI KAZI CHA TAIFA KWA AJILI YA KUANGALIA ATHARI ZA UCHUMI ZINAZOTOKANA NA UGONJWA WA CORONA


Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Bunge, Freeman Mbowe, ameshauri  kuundwa kwa kikosi kazi cha Taifa kwa ajili ya kuangalia athari za uchumi za ugonjwa huo.

Mbowe aliyasema hayo jana April 6, 2020  wakati akichangia Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka 2020/21.

Alibainisha kuwa sekta ya utalii imeanguka kwa asilimia 99 na kwamba kuna makampuni yamefungwa huku mapato ya nchi yatapungua kwa asilimia 40 kwa miezi sita ijayo.

“Kumekuwa na kauli tofauti,mikusanyiko ambayo haifai na kwamba kuna mikusanyiko ambao wakuu wa mikoa ndio wamekuwa wakiifanya, wanakusanya watu, wanahutubia watu kwamba ugonjwa uko mbali hii ni hatari,”amesema.

Aliongeza “Ningetamani tumsikilize Rais, Waziri Mkuu na Waziri wa Afya kama nchi ikienda kwa kila kiongozi kutoa taarifa ugonjwa huu utawafikisha mahali pabaya.”

Alisema jambo hilo linahitaji kikosi cha Taifa kwa ajili ya kuangalia athari za uchumi na kijamii na pia kuangalia vipaumbe vya Taifa hivi sasa ni vipi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post