MBWANA SAMATTA AVUNJA REKODI KWA KUFUNGA GOLI MOJA MATATA


Mbwana Samatta amefunga bao lake la kwanza kwenye Uwanja wa Wembley  kunako Dakika ya 41 wakati Aston Villa ikivaana na Manchester City katika fainali ya Kombe la Carabao.


Nahodha huyo  wa Tanzania ameanza katika kikosi cha kwanza cha Aston Villa na kazi yao ni moja tu.... kuhakikisha wanawazuia Manchester City kutetea ubingwa wake wa Kombe la Carabao.


Villa mara ya mwisho kutwaa ubingwa ilikuwa msimu wa 1995/96 .

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527