KENYA YATHIBITISHA KIFO CHA KWANZA CHA MGONJWA WA CORONA


Mgonjwa wa kwanza mwenye maambukizi ya virusi vya corona (covid-19) nchini Kenya amefariki katika Hospitali ya Aga Khan.

Taarifa hiyo  imethibitishwa na Waziri wa Afya nchini humo, Mutahi Kagwe ambaye amesema mgonjwa huyo ni mwanaume aliyekuwa na umri wa miaka 66 na alikuwa amelazwa Katika Chumba cha Uangalizi Maalum (ICU).

“Mwanaume huyo pia alikuwa na ugonjwa wa sukari na alikuja nchini Machi 13, 2020 kutoka Afrika Kusini akipitia Swaziland,” imesema taarifa hiyo.

Kenya hadi sasa imeripoti kesi za Corona 31 tangu kutangaza mgonjwa wa kwanza Machi 13, 2020.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527