NYAMAPORI SASA KUUZWA KIHALALI KWENYE MABUCHA


Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imepitisha kanuni za kuanzisha mabucha ya nyamapori, na pia imerekebisha kanuni za uanzishaji bustani, mashamba, na ranchi za wanyamapori.



Hayo yamesemwa leo Jumapili (Februari 9, 2020) na Waziri Hamis Kigwangalla kupitia ukurasa wake wa Twitter ambapo amewataka Watanzania kuchangamkia fursa hizo za kuichumi za kuuza nyama za wanyamapori kihalali pamoja na kufungua bustani za maonesho ya wanyamapori.

Kigwangalla amesema kuwa kupitia ridhaa iliyotolewa na Rais John Magufuli sasa mwananchi mwenye hamu na nyamapori anaweza kuipata kihalali.

“Tuliahidi kuanzisha mabucha ya nyamapori, tumetekeleza. Tunamshukuru sana Mhe. Rais Dr. John Pombe Magufuli kwa kutoa ridhaa yake tuweze kufanya hivi. Sasa ukiwa na hamu ya nyamapori utaweza kuipata kihalali. Wajasiriamali hii nayo ni fursa mpya, changamkieni,” ameandika Kigwangalla.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post