MWANAJESHI MWINGINE WA UTURUKI AUAWA KWA BOMU NA VIKOSI VYA SYRIA VINAVYOUNGWA MKONO NA URUSI


Askari mwingine wa Uturuki ameuawa kwenye shambulio la bomu katika mkoa wa Idlib. 

Huyo ni askari wa 16 kuuawa kwenye mashambulio yanayofanywa na vikosi vya Syria vinavyoungwa mkono na Urusi. 

Wizara ya ulinzi ya Uturuki imesema mauaji hayo yametokea wakati ambapo mazungumzo ya kusitisha mapigano baina ya Ankara na Moscow yamekwama. 

Kuongezeka kwa vifo vya wanajeshi wa Uturuki, kunaweza kuondoa uwezekano wa kupatikana suluhu ya kusitisha mapigano katika eneo la Kaskazini magharibi mwa Syria. 

Tangu mapema mwezi Desemba, raia karibu milioni moja wa Syria wengi wao ni wanawake na watoto hawana makaazi na hasa katika kipindi hiki cha baridi kutokana na mapigano. 

Rais wa Uturuki Tayyip Erdogan anatarajia kukutana na viongozi wenzake wa Urusi, Ujerumani na Ufaransa Machi 5 kwa ajili ya kuuzungumzia mkoa wa Idlib.

Baada ya syria kukumbwa na vita kwa miaka tisa sasa, vikosi vya serikali ya Syria vinapambana kulidhibiti eneo hilo la mwisho linaloshikiliwa na waasi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post