JAJI KUFUNGULIWA MASHITAKA KWA KUDAIWA KUSHIRIKIANA NA MSHUKIWA WA MAUAJI

Jaji mmoja nchini Kenya anayejulikana kwa jina la Sankale Ole Kantai atafunguliwa mashtaka Mahakamani kufuatia madai kwamba alishirikiana na mshukiwa wa mauaji.

Jaji huyo wa Mahakama ya rufaa, Sankale Ole Kantai alikamatwa na maafisa wa jinai siku ya Ijumaa na kuhojiwa kuhusu uhusiano wake wa karibu na Sara Waimu , mshukiwa mkuu wa mauaji ya raia wa Uholanzi Tob Cohen.

Jaji huyo aliachiliwa siku ya Jumamosi mchana kwa dhamana baada ya kulala katika kituo cha polisi cha Muthaiga ambapo alikuwa anazuiliwa. Atawasilishwa mahakamani siku ya Jumanne.

Idara ya Jinai imethibitisha kwamba jaji huyo atafunguliwa mashtaka ya kuwa na njama ya kuilaghai haki na kuingilia mashahidi.

Mwili wa raia huyo tajiri kutoka Uholanzi ulipatikana katika shimo la maji taka nyumbani kwake jijini Nairobi 2019.

Kwa mujibu wa BBC, Maafisa wa polisi wanasema kwamba wana sababu za kuamini kwamba jaji Sankale alikuwa na uhusiano wa karibu na mshukiwa huyo ambaye amedaiwa kumpa ushauri ili kukabiliana na kesi yake mahakamani.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527