RAIS MSTAAFU AJIUA KWA KUJIPIGA RISASI


Rais wa zamani wa Peru, Alan García.

Rais wa zamani wa Peru, Alan García amejipiga risasi mwenyewe, baada ya kugundua kuwa anatafutwa na jeshi la polisi nchini humo kwa kosa la kupokea rushwa.

García anatuhumiwa kwa kuchukua rushwa kutoka kampuni ya ujenzi wa Brazil Odebrecht, ambapo amekuwa akizikataa tuhuma hizo mara kwa mara.

Luis Gonzales Posada, ambaye ni mmoja kati ya viongozi wa chama cha García, amesema hali yake ni mbaya, "hebu tumuombee Mungu kumpa nguvu," aliwaambia waandishi wa habari hospitali.

García ambaye alikuwa Rais kuanzia mwaka 1985 hadi 1990 na kurudi madarakani tena mwaka 2006 hadi 2011.

Taarifa zilizotolewa na wachunguzi zinadai kuwa, yeye alichukua rushwa kutoka Odebrecht wakati wa kipindi cha pili cha Urais ambapo Odebrecht amekubali kulipa karibu $ 30m (£ 23m) kama rushwa nchini Peru tangu 2004.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post