AJIUZULU UBUNGE BAADA YA KUIBA MKATE




Darij Krajcic.
Mbunge mmoja nchini Slovenia amejiuzulu baada ya kuiba mkate maarufu 'Sandwich' katika duka moja kwa madai kuwa wahudumu wa sehemu hiyo walimpuuzia.

Darij Krajcic ameviambia vyombo vya habari vya ndani kuwa alipuuzwa na wafanyakazi wa duka hilo na walikuwa wakiendelea na shughuli zao na hakujulikana kama ameiba lakini baadae baadhi ya wanachama walisisitiza arudi kulipa pesa ya mkate huo.

''Nilisimama pale kwa dakika tatu, nikitaka wanihudumie", alijitetea Mbunge huyo.

Krajcic ameomba msamaha na kusema kuwa anajutia kitendo alichokifanya, baada ya suala lake la kuiba kusambaa baada ya kuwaambia wabunge wengine wakati wa mkutano wa kamati siku ya Jumatano ambapo siku ya Alhamisi spika wa bunge hilo Brane Golubovic, alikemea vikali kitendo cha mbunge kuiba, na kusema kuwa ni kitendo kisichokubalika.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527